Jumatatu, 19 Septemba 2011

Je Unajua Kama Kuna Mbinu za Kutajirika?


Kuna NGUVU ambayo kila kitu kiliumbwa kutoka  kwake, ambacho kwa asili yake inaruhusu, inapitisha na kuujaza uwazi ulioko katika ulimwengu. 

Wazo linalokuwa katika NGUVU hiyo huzalisha kitu ambacho kimefikiriwa katika wazo hilo. 

Mtu anaweza kutengeneza wazo lake na kwa kuliweka katika NGUVU hiyo isiyokuwa na umbo anaweza kusababisha kitu anachokifikiri kutengenezwa. 

Ili kuweza kufanya haya, mtu lazima atoke katika hali ya ushindani na aingie katika hali ya ufahamu wa ubunifu. Bila hivyo hawezi kwenda sambamba na NGUVU hiyo ambayo siku zote ni bunifu na wala haina roho ya ushindani.  

Mtu anaweza kwenda sawa na NGUVU hii kwa kuwa na shukurani ya kweli kwa baraka ambazo amewahi kupata. Shukurani huunganisha ufahamu wa mtu na akili ya NGUVU ili wazo la mtu liweze kupokelewa na NGUVU hiyo.

Mtu anaweza kubaki katika hali ya ubunifu kama tu akijiunganisha na akili ya NGUVU kupitia hisia za ndani na za siku zote za shukurani. 

Mtu anaweza kutengeneza picha ya vitu anavyotaka kuvipata, kuvifanya au unavyotaka kuwa na ni lazima kushikiria picha ya vitu hicho katika mawazo yake na kuwa na shukurani za ndani kwa NGUVU kwamba amepata hitaji lake. Mtu anayetaka kuwa kuwa tajiri lazima atumie muda wake kufikiria ndoto yake na shukurani kuwa amepokea kile anachokitaka.


Umewahi kuona watu wa elimu sawa, mazingira sawa, biashara sawa na kila kitu kiko sawa, lakini mmoja anakuwa tajiri mwingine fukara wa kutupwa? Au umewahi kuona wale waliokuwa na akili sana darasani wanakuwa masikini huku mbumbumbu wa kutupwa anakuwa tajiri? 

Kuna sayansi na njia sahihi za kuwa tajiri. Hizi zikifuatwa kwa usahihi lazima mtu atakuwa tajiri. Haihitaji uwe New York au London au Paris au kokote walikoendelea ndiyo uwe tajiri. Ndiyo maana hata huko kuna masikini wakubwa wakati Tanzania pia kuna mabilionea na masikini. Hata jagwa la sahara pamoja na ukame kuna matajiri pia. Hivyo kuna mbinu za kuwa tajiri.

Hivyo ni jukumu la kila mtu kujifunza mbinu hizi na sayansi ya kupata utajiri. Elizabethrose Memorial Institute imedhamiria kufundisha wajisiriamali njia sahihi za kupata mafanikio BURE. Maana tunaamini ili kufanikiwa lazima usaidie wengi. Wasiliana wasi tukusaidie.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni