Jumapili, 9 Februari 2014

Njia Mpya ya Kuuza Bidhaa za Makampuni ya Network Marketing


Umewahi kusikia makampuni kama Forever Living Products, GNLD, Amway, Empower Network, DSDomination n.k ambayo huuza bidhaa zake kwa njia y mtandao yaani Network Marketing. Makampuni ambayo ni maarufu hapa Tanzania ni Forever Living na GNLD. Makampuni haya huuza bidhaa zitokanazo na mimea na huuza kwa njia ya mtandao (Network).

Network Marketing ni njia ya kuuza bidhaa ambayo imekuwapo tangiu miaka mingi. Biashara ya network inataka mtu ajiunge kwenye kampuni na kununua bidhaa za kuanzia. Mara nyingi inatakiwa bidhaa hizo uzitumie kwanza na zingine uziuze. Kutumia bidhaa hizo inakupa uelewa wa jinsi zilivyo nzuri na zinavyosaidia matatizo ya watu. Baada ya kuziuza na kutumia unatakiwa uanze kutafuta watu ambao watajiunga na kampuni na wao kuanza kuuza bidhaa hizo. 

Kwa kila mtu anayejiunga, aliyemuingiza hupata kamisheni na bidhaa atakayouza utapata pasenti fulani ya mauzo hayo. Chukulia kwa mfano, umeingiza watu watano, kila uliyemuingiza utapata kamisheni, na kila bidhaa itakayouzwa na watuwako uliowaingiza utapata pasenti ya mauzo hayo. Ndiyo maana inaitwa biashara mtandao.

Faida kubwa ya  kujiunga n makampuni haya ni kuwa mtu anakuwa na biashara yake na kisha anaweza kuifanya akiwa nyumbani kwake bila kukutana na bosi wala foleni za kila siku za mjini. Anajipangia muda wa kufanya kazi na muda wa kupumzika. 

Kampuni hizi zilivyoingia nchini zilipokelewa vizuri sana na watu walianza kutumia bidhaa zake sambamba na kujiunga kama wasambazaji. Hata hivyo biashara hizi zimeendelea kupungua umaarufu wake. Tumefanya utafiti wa haraka kwa nini watu hawajiungi sana na makampuni haya.


 Sababu ambazo watu wengi wanatoa ni kuwa hawezi kutembeza biashara kutoka nyumba hadi nyumba, au maofisini kutafuta wateja. Pia kuna hii mikutano y majumbani ya kualika ndugu na marafiki na kuwaelezea biashara, inaonekana kutowafurahish walio wengi.  Kwa ujumla njia zinazotumika kuuza na kuingiza wasambazaji ndiyo hasa zimeshusha hamasa ya walio wengi kujiunga.

Kwa kuzingatia sababu hizi, sisi JCM Marketing Coach tumebuni njia rahisi ya nyepesi ya kuuza na kuhamisisha waliowengi kujiung kama wasambaji. Njia hizi hazihitaji upigie watu 100 simu kila wakati, hakuna tena kuzunguka maofisi na kubembeleza watu wanunue bidhaa zako, hakuna mikutano ya majumbani na mahoteli tena. 

Kama unataka kujiunga na biashara hizi n kujifunza mbinu mpya za kuuza bidhaa hizi tafadhali wasiliana nasi. Pia usiache kutoa maoni yako hapo chini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni