Alhamisi, 25 Agosti 2011

Walioko Nyuma ya EMI

Enock Mayage :CPA (T), Msc in Auditing and Consultancy (UK).
Mayage amejikita sana katika kuwafundisha wajasiriamali wanaoanza na wale ambao tayari wameanza. Ni mtalaam wa fani ya uhasibu na ukaguzi wa mahesabu na ushauri, utalaam aliousomea nchini Uingereza. Pia amejikita katika kuhamasisha na kutia moyo juu ya maisha na ubunifu wa biashara. Amekuwa mzungumzaji (public speaker) katika makongamano ya ndani na nje ya nchi juu ya biashara na mafanikio. Mayage anaamini mtu yeyote anaweza kupata kile anachokitaka. Mafundisho haya yanasimama kwenye kanuni iliyotumiwa na akila Henry Ford, Edson, Oprah, Anderson, John Assaraf, Bob Proctor, Jim Rohn, Tony Robins na wengine kujipatia mafanikio makubwa. Falsafa zinazotumika katika mafunzo haya ni za watu mashuhuri duniani kama akina Nelson Mandela, M.Ghandi, JK Nyerere, F.Kennedy n.k ambao waliamini kuwa ukitaka kufanikiwa saidia kwanza wengi.

Herieth K. Mushi
Ni Meneja na Masoko wa Tasisi. Amefanya kazi na Tasisi kwa muda mrefu kwa kuwasaidia wateja wengi katia biashara zao. Herieth pia ameakuwa mzungumzaji wa maswala ya ujasiriamali ambapo amewasaidia wengi kubadilisha mitazamo yao juu ya maswala ya ujasiriamali. Pia amewahi kufanya kazi na mashirika mbalimbali za kitaifa na kimataifa yanayojihusisha na ujasiriamali kama vile Shirika la Umoja wa Mataifa na Maendeleo ya Viwanda na Biashara (UNIDO) katika mradi wa Africa Investor Survey.

Regina E. Pandisha
Ni Msaidizi wa Mtendaji Mkuu. Amekuwa na Tasisi kwa muda
mrefu. Ni mzoefu na mzungumzaji wa maswala ya ujasiriamali. Regina ameandaa mikutano mingi ya wajasiriamali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni